Kwanini Unafeli Mtandaoni

Written by Shukuru Amos

I am the founder of Tanzlite Digital, Creator, Author of Mbele Ya Muda, and the most followed Tanzanian marketer on LinkedIn.

Posted September 2, 2024

Hebu tuwe wakweli Kuhusu Kupata Wateja Mtandaoni . Tangu uamue kuuza maarifa mtandaoni hakuna kilichotokea. Juhudi za kupost na kucomment kila mara zinaishia kuwa mbuzi wa masikini –hazizai matunda. Watu hawakufuati kutaka huduma yako.

DM yako ni kavu kama jangwa la Kalahari. Hadhira uliyonayo (followers) hawakufuatilii. Likes na comments ni za kumulika kwa tochi. Hata Likes zikiwa nyingi, bado mauzo ni sifuri.

Mbaya zaidi, hata haujui kwanini unafeli mtandaoni. Haujui shida iko wapi!

Ukweli ni kwamba huna hadhira inayokuchukulia serious. You don’t have an audience.

Jina lako mtandaoni halina hadhi, hujaweza kujitofautisha na ndiyo maana watu hawaoni sababu kwanini wakuchague wewe. You are just another voice in the noise.

Hii makala itakusaidia sana.

Nimeamua kuandika kitu ambacho utakifanyia kazi papo na kuanza kona mabadiliko.

Twende kazi!

Shida ya kwanza: Huna kitu kinaitwa “narrative”

Kosa kubwa unaloweza kulifanya mtandaoni ni kuingia bila kuwa na simulizi inayokutambulisha. Hapa siongelei historia ya maisha yako sijui wewe ni nani, ulizaliwa wapi ikaja ikaenda….hapana. Hiyo ni sehemu tu ya kuunda narrative.

Kuwa na narrative maana yake ni ule mjumuiko wa stori, mawazo na vitendo vinavyojenga taswira yako ya kipekee. Mambo gani unasimamia, yapi unayapinga —yaani how are your choices, values and action build up a narrative around your identity?

Unataka mfano? Sawa.

Tuseme haupendi kuajairiwa, ulijaribu ukaacha kazi na sasa uko na mishe zako binafsi (Solopreneurship).Kwahiyo narrative yako itakuonyesha kama mtu anayependa uhuru na ni mjasiriamali. 

Mfano mwingine wa kuunda narrative yako ni kuunda misemo yako na namna pekee ya uwasilishaji. Yaani hautumii maneno na lugha iliyozoeleka kwenye niche yako.

Hakikisha una “kaongelee” kako, misemo yako, misimamo na mitindo yako.

Hakikisha una kaongelee kako, misemo yako, misimamo na mitindo yako.

Shukuru Amos

Kwa mfano mimi; nina misemo na misimamo yangu maarufu kule LinkedIn:

  • “Kataa Fikra Elekezi”
  • “Social Rhetoric”
  • “Content Alchemist”
  • “Holiday posts are useless”
  • “Awards are useless” 

Usitumie msamiati wao. You’re not just another corporate person using corporate verbatim.

Kama kila mtu kwenye B2B anasema yeye ni “Best au award winning service provider” basi kaa mbali na utambulisho wa namna hiyo. Toka kivingine. Utofauti unakumbukwa. Utofauti unakaa akilini.

Shida ya pili: Una Uoga na Aibu

Tatizo lingine linalopelekea kufeli mtandaoni ni kwamba huna ujasiri wa kuongea kwa sauti yenye mamlaka. You’re being too safe. And shy.

Acha kuremba maneno unapoongelea upuuzi unaofanyika in your niche. Even worse, umeingia kwenye niche fulani na ukafanana na wote walio kwenye hiyo niche. 

Sasa nani akusikilize ikiwa umeingia na kuwa kama uliowakuta?

Be a contrarian. Kosoa kile ambacho wengi wanakiamini kwa kuonyesha ama kiko overrated au ni simply useless. Kataa Fikra Elekezi zilizomo kwenye tasnia hiyo.

Hivyo ndiyo utaweza kuonekana na kuchukuliwa serious.

Shida ya tatu: watu hawajali

Umeingia mtandaoni ukijua unachokijua. Lakini hujakaa kudadavu ni kina nani hasa unawalenga. Wanahitaji nini? Kipi kinawakosesha usingizi?

Usiwe tu na hadhira ya jumla, ni lazima uchimbe mpaka umpate unayemtaka.

Kama uko kwenye fitness, unaweza kuamua unataka kuhudumia wanaume au wanawake? Pengine ukaenda niche zaidi ukasema fitness coach for stay home moms, au fitness coach for busy female corporate workers.

Shida ya nne: Maudhui yako yanaboa

Hii ni changamoto ya uwasilishaji. Uandishi wako hauna ladha, hauna vichombezo shirikishi kama vile misemo na tamathalli semi. Yaani unawasilisha tu ilimradi.

Kama ni video basi usemaji, mazingira na vielelezo vya mwili havivutii.

Shida ya 5: Hauko serious

Hapa kuna mambo mawili; bidii na kujigharamia kuwa bora. 

Nikuulize swali, ndani ya miezi 9 iliyopita umewahi kulipia maarifa? Yaani kununua kitabu, course, coaching session. Au paid subscription kama vile Medium Membership, X Pro, newspaper subscription n.k. Kama jibu ni hapana au haukumbuki basi hauko serious.

Kuhusu bidii: Kama mwezi huu unajaribu, mwezi ujao hatukuoni; halafu baada ya muda unakuja tena unafanya fanya unapotea tena. Hapa si bora utafute ajira na ukawe mfanyakazi mtiifu. Mafanikio mtandaoni yanahitaji watu wanaojituma.

Kama haujui kinachokufanya usifanikiwe mtandaoni, hauwezi kupata suluhu. Kama haujui ni aina gani ya maudhui yanafanya vizuri, utaendelea kubahatisha.

Nina matumanini makala hili imekufanya uhoji mkakati wako mzima wa kuuza maarifa mtandaoni.

Ninaitwa Shukuru Amos. Ni mwandinshi wa kitabu cha Mbele Ya Muda. Ndani ya hiki utajifunza kuhusu personal branding, maudhui na biashara mtandaoni. Pia nimeandika Mwongozo mfupi kukusaidia Kutengeza Profile Yako ya LinkedIn au X mwanzo mwisho. 

Mwisho

Unaishi kwenye Ulimwengu wa Digitali. LAKINI kwanini habari za kupata PESA na MAFANIKIO Mtandaoni unazisikia kwa watu wengine tu? Na ukiangalia bado KIJANA kabisa. Ni kweli umekubali kuwa mtazamaji kwenye Uchumi wa DIGITALI? Hapana bwana!

1 Comment

  1. Andrew Peter Kato

    Ahsante sana for this Food for Thought!

    Reply

Submit a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.

Governments vs Social Media: Build That Website

Governments vs Social Media: Build That Website

It is not a wise idea to put all your eggs in one basket. Especially if you have little ownership of that basket. Recent feuds between governments and social media giants highlight the risks of relying on third-party platforms for business. Here’s why owning your...

Introducing Tanzlite Host: The New Web Hosting Player in Tanzania

Introducing Tanzlite Host: The New Web Hosting Player in Tanzania

Earlier this year, we introduced Tanzlite Host. This is not just another name in Tanzania's web hosting services; we're rewriting the rules. Here's how our unique approach to business is setting us apart and why it's the most profitable model in the industry: A...

Products From Tanzlite